"Tulichukua njia ya mkato kuelekea nyumbani. Sikuona dalili zozote kuwa Maria anamtambua Idda, nami nikajipongeza... "Willy niliiweka roho yangu mikononi mwako nilipoamua kuishi nawe, lakini kwa sababu umeshindwa kuitunza vizuri nimeamua kuirudisha." Laiti mtu angelijua harufu ya mauti yake basi angeyakimbia kila yanapotaka kumfikia. Lakini kwa kuwa mwanadamu hatambui kuwa matendo yake na mwelekeo wa maisha ndiyo huwa harufu ya mauti yake, hujikuta amenaswa na mauti bila kutarajia.